Thursday, December 31, 2009

Happy New Year... Heri ya Mwaka mpya na kwaheri 2009

Today I would like to share this poem written in Swahili by a talented young man studying in Turkey. An Eulogy to 2009.

NAONDOKA!
>
>
> Shairi naliandika, Natumai mko poa
> Izraili amefika, Roho yangu kuitoa
> Mwito kifo naitika, Meshindwa kujiokoa
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
> Ni miezi na masiku, Nami nimevumilia
> Nakumbuka ile siku, Nilipo waingilia
> Tena mida ya usiku, Nyote mkasubiria
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Saa zenu kwa pamoja, MlifUata akrabu
> Kwa sekunde mojamoja,Mkaweza kuhesabu
> Nne tatu mbili moja, Mkanambia karibu
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Hoye mkafurahia, Kwa shangwe mkanilaki
> Tena mkashangilia, Mukawasha mafataki
> Kwa masoda na mabia, Hakuna kilichobaki
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Awali mlinipenda, Na wala hamukugomba
> Elfu mbili na kenda,Kwenu ni mgeni bomba
> Ili nisiweze kwenda, Kukicha mkaniomba
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Tumekuwa marafiki, Wa kufa na kuzikana
> Tulogawana riziki, Wala hatukunyimana
> Hasa wakati wa dhiki,Daima tulifaana
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Vipi leo mwachukia, Kunilani kwa matusi
> Tangu nilipoingia, Ni mafua na virusi
> Mwatamani nifukia, Mpate ondoa nuksi
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Serikali zalalama, Mgeni mie sifai
> Uchumi umeshazama, Benki zinawadai
> Bidhaa zote gharama, Mpaka mumenikinai
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Namaliza msafara, Nilikuwa tu mgeni
> Mliopata madhara, Mtapata afueni
> Mliokula hasara, Nasema tena poleni
> Hata hivyo yote tisa, Kumi mie naondoka
>
>
>
>
> Hivi sasa nawatoka, Bora tu niwaacheni
> Kuwa nanyi nimechoka,Kwaheri nawaageni
> Sina budi kuchomoka, Yupo mwengine mgeni
> Hata hivyo yote tisa, Kumi roho yanitoka
>
>
>
>
> Mpokeeni mwenzangu, Anayefanana nami
> Jina lake kama langu,Elfu mbili na kumi
> Tabia ni kama zangu, Msimpige mangumi
> Hata hivyo yote tisa, Kumi roho yanitoka
>
>
>
>
> Kiumri nimemzidi, Hawezi kutabirika
> Basi namujitahidi, Kabla yeye kufika
> Mabadiliko yabidi, Msije kuathirika
> Hata hivyo yote tisa, Kumi roho ishatoka
>
>
>
>
>
> HAMZA A. MOHAMMED a.k.a 2009
>

No comments: